Sunday, June 20, 2010

UMESIKIA HII?

Wanariadha wapatao 30 kati ya mamia waliojitokeza katika mashindano ya mbio kusaka wanariadha 100 wa mwanzo watakaojiunga na chuo kikuu cha michezo nchini China wamebainika kufanya udanganyifu kwa kupita njia za panya. Miongoni mwa mbinu walizotumia ni kupanda lifti za magari na kukodi wakimbiaji wa kasi, shirikisho la mchezo huo nchini humo lilisema baadhi ya watu wanaoshiriki mashindano hayo maarufu kama Xiamen International Marathon katika jimbo la kusini mashariki mwa Fuji kuwa watu hao walifanya udanganyifu huo kwa ajili ya kuwa katika nafasi za mwanzo ili wachukuliwe na chuo hicho. China wamekuwa maarufu sana duniani kwa kuingiza bidhaa zisizo na ubora sokoni (bidhaa feki).

No comments:

Post a Comment