Monday, September 27, 2010

IJUE INJINI YA DIZEL

Mafuta ya kuendeshea mitambo mikubwa na injini za magari (Dizel) ni mafuta mazito na hufaa kwa injini kubwa ili kupunguza matumizi makubwa ya mafuta yaani tofauti na mafuta ya Petrol ambayo ni mepesi zaidi na ni bora kwa injini ndogo, hasa za magari madogo, pikipiki na mashine nyingine kama jenereta ndogo. Je unajua kama injini ya Dizel huwa ni nzito zaidi ya injini ya Petrol, na je unajua kama injini ya Dizel huwa ina tabia ya kutetemeka zaidi inapokuwa imefugwa katika bodi ya gari? Na unajua kuwa kutetemeka kwa injini hiyo uchangia kuchosha mabodi ya magari hasa magari madogo.

1 comment: